- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi94
Listen to this chapter
0:00
0:00
Ombi la Kisasi na Haki ya Mungu
1
Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
2
Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
3
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
4
Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
5
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
6
Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
7
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
Onyo kwa Wapumbavu Wanaokandamiza
8
Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
9
Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
10
Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
11
Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
Heri ya Nidhamu ya Mungu
12
Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,
13
unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu.
14
Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake.
15
Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata.
Kumtumaini Bwana, Mtetezi
16
Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu?
17
Kama Bwana asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.
18
Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia.
19
Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.
20
Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake?
21
Huungana kuwashambulia wenye haki, kuwahukumu kufa wasio na hatia.
22
Lakini Bwana amekuwa ngome yangu, na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia.
23
Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; Bwana Mungu wetu atawaangamiza.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note