- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi85
Listen to this chapter
0:00
0:00
Kukumbuka Wokovu wa Mungu wa Zamani
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana, ulionyesha wema kwa nchi yako. Ulimrejeshea Yakobo baraka zake.
2
Ulisamehe uovu wa watu wako, na kufunika dhambi zao zote.
3
Uliweka kando ghadhabu yako yote na umegeuka na kuiacha hasira yako kali.
Ombi la Kurejeshwa Sasa
4
Ee Mungu Mwokozi wetu, uturejeshe tena, nawe uiondoe chuki yako juu yetu.
5
Je, utatukasirikia milele? Utaendeleza hasira yako kwa vizazi vyote?
6
Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wakufurahie?
7
Utuonyeshe upendo wako usiokoma, Ee Bwana, utupe wokovu wako.
Uhakika wa Amani ya Mungu
8
Nitasikiliza lile atakalosema Mungu aliye Bwana; anaahidi amani kwa watu wake, watakatifu wake: lakini nao wasirudie upumbavu.
9
Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao, ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.
10
Upendo na uaminifu hukutana pamoja, haki na amani hubusiana.
11
Uaminifu huchipua kutoka nchi, haki hutazama chini kutoka mbinguni.
12
Naam, hakika Bwana atatoa kilicho chema, nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.
13
Haki itatangulia mbele yake na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note