Rukia maudhui

Zaburi85

Kukumbuka Wokovu wa Mungu wa Zamani

1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana, ulionyesha wema kwa nchi yako. Ulimrejeshea Yakobo baraka zake.
2
Ulisamehe uovu wa watu wako, na kufunika dhambi zao zote.
3
Uliweka kando ghadhabu yako yote na umegeuka na kuiacha hasira yako kali.

Ombi la Kurejeshwa Sasa

4
Ee Mungu Mwokozi wetu, uturejeshe tena, nawe uiondoe chuki yako juu yetu.
5
Je, utatukasirikia milele? Utaendeleza hasira yako kwa vizazi vyote?
6
Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wakufurahie?
7
Utuonyeshe upendo wako usiokoma, Ee Bwana, utupe wokovu wako.

Uhakika wa Amani ya Mungu

8
Nitasikiliza lile atakalosema Mungu aliye Bwana; anaahidi amani kwa watu wake, watakatifu wake: lakini nao wasirudie upumbavu.
9
Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao, ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.
10
Upendo na uaminifu hukutana pamoja, haki na amani hubusiana.
11
Uaminifu huchipua kutoka nchi, haki hutazama chini kutoka mbinguni.
12
Naam, hakika Bwana atatoa kilicho chema, nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.
13
Haki itatangulia mbele yake na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options