- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi41
Listen to this chapter
0:00
0:00
Baraka za Kuwahurumia Wanaoteseka
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2
Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3
Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Maombolezo na Maombi ya Daudi
4
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Ombi la Ujasiri la Wokovu wa Mungu
10
Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11
Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12
Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
Sifa: Hitimisho la Kitabu cha Kwanza
13
Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note