Rukia maudhui

Zaburi13

Kilio cha Kuachwa

1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpaka lini, Ee Bwana? Je, utanisahau milele? Utanificha uso wako mpaka lini?
2
Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda mpaka lini?

Ombi la Mungu Kuingilia

3
Nitazame, unijibu, Ee Bwana Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4
Adui yangu atasema, “Nimemshinda,” nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.

Kugeukia Tumaini na Sifa

5
Lakini ninategemea upendo wako usiokoma; moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6
Nitamwimbia Bwana, kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options