Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Sun: Created

8 mistari · 8 vipengele

Mistari kuhusu Created

  1. Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe usiku na mchana, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbalimbali, siku na miaka,

  2. nayo iwe mianga kwenye nafasi ya anga ya kutia nuru juu ya dunia.” Ikawa hivyo.

  3. Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota.

  4. Mungu akaiweka katika nafasi ya anga iangaze dunia,

  5. itawale usiku na mchana, na ikatenganishe nuru na giza. Mungu akaona kuwa hili ni jema.

  6. Mchana ni wako, nao usiku ni wako pia, uliziweka jua na mwezi.

  7. Ambaye aliumba mianga mikubwa, Fadhili zake zadumu milele.

  8. Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyeweka jua liwake mchana, yeye anayeamuru mwezi na nyota kungʼaa usiku, yeye aichafuaye bahari ili mawimbi yake yangurume; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake: