Mistari ya Biblia kuhusu Darkness
Mistari muhimu ya Biblia
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,