Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Ahira

9 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”

  2. Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.

  3. Siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa watu wa Naftali, alileta sadaka yake.

  4. Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;

  5. sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;

  6. fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;

  7. mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;

  8. maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani.

  9. naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.