Skip to content
Zaburi 98:4-9

Zaburi 98:4-9

4
Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote, ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;
5
mwimbieni Bwana kwa kinubi, kwa kinubi na sauti za kuimba,
6
kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume: shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme.
7
Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake, dunia na wote wakaao ndani yake.
8
Mito na ipige makofi, milima na iimbe pamoja kwa furaha,
9
vyote na viimbe mbele za Bwana, kwa maana yuaja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki na mataifa kwa haki.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options