Zaburi 90:3-9
3
Huwarudisha watu mavumbini, ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”
4
Kwa maana kwako miaka elfu ni kama siku moja iliyokwisha pita, au kama kesha la usiku.
5
Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo, nao ni kama majani machanga ya asubuhi:
6
ingawa asubuhi yanachipua, ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.
7
Tumeangamizwa kwa hasira yako na tumetishwa kwa ghadhabu yako.
8
Umeyaweka maovu yetu mbele yako, dhambi zetu za siri katika nuru ya uwepo wako.
9
Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako, tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza.
Settings