Skip to content
Zaburi 90:3-10

Zaburi 90:3-10

3
Huwarudisha watu mavumbini, ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”
4
Kwa maana kwako miaka elfu ni kama siku moja iliyokwisha pita, au kama kesha la usiku.
5
Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo, nao ni kama majani machanga ya asubuhi:
6
ingawa asubuhi yanachipua, ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.
7
Tumeangamizwa kwa hasira yako na tumetishwa kwa ghadhabu yako.
8
Umeyaweka maovu yetu mbele yako, dhambi zetu za siri katika nuru ya uwepo wako.
9
Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako, tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza.
10
Siku zetu za kuishi ni miaka sabini, au miaka themanini ikiwa tuna nguvu, lakini yote ni ya shida na taabu, nazo zapita haraka, nasi twatoweka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options