Zaburi 9:7-12
7
Bwana anatawala milele, ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.
8
Mungu atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kwa haki.
9
Bwana ni kimbilio la watu wanaoonewa, ni ngome imara wakati wa shida.
10
Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe, kwa maana wewe Bwana, hujawaacha kamwe wakutafutao.
11
Mwimbieni Bwana sifa, amefanywa mtawala Sayuni, tangazeni miongoni mwa mataifa, yale aliyoyatenda.
12
Kwa maana yeye alipizaye kisasi cha damu hukumbuka, hapuuzi kilio cha wanaoonewa.
Settings