Skip to content
Zaburi 9:1-6

Zaburi 9:1-6

1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa muth-labeni. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote, nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
2
Nitafurahi na kushangilia ndani yako. Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.
3
Adui zangu wamerudi nyuma, wamejikwaa na kuangamia mbele zako.
4
Kwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu; umeketi kwenye kiti chako cha enzi, ukihukumu kwa haki.
5
Umekemea mataifa na kuwaangamiza waovu; umeyafuta majina yao milele na milele.
6
Uharibifu usiokoma umempata adui, umeingʼoa miji yao; hata kumbukumbu lao limetoweka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options