Zaburi 9:7-10
7
Bwana anatawala milele, ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.
8
Mungu atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kwa haki.
9
Bwana ni kimbilio la watu wanaoonewa, ni ngome imara wakati wa shida.
10
Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe, kwa maana wewe Bwana, hujawaacha kamwe wakutafutao.
Settings