Rukia maudhui
Zaburi 78:12-16

Maajabu ya Mungu Nyikani

Zaburi 78:12-16
12
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options