Zaburi 7:1-5
1
Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini. Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe, uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
2
la sivyo watanirarua kama simba na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
3
Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya na kuna hatia mikononi mwangu,
4
au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
5
basi adui anifuatie na kunipata, auponde uhai wangu ardhini na kunilaza mavumbini.
Settings