Zaburi 66:17-20
17
Nilimlilia kwa kinywa changu, sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
18
Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, Bwana asingekuwa amenisikiliza;
19
lakini hakika Mungu amenisikiliza na amesikia sauti yangu katika maombi.
20
Sifa apewe Mungu, ambaye hakulikataa ombi langu wala kunizuilia upendo wake!
Settings