Ushuhuda Binafsi wa Sala Iliyojibiwa
16
Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu, nami niwaambie aliyonitendea.
17
Nilimlilia kwa kinywa changu, sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
18
Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, Bwana asingekuwa amenisikiliza;
19
lakini hakika Mungu amenisikiliza na amesikia sauti yangu katika maombi.
20
Sifa apewe Mungu, ambaye hakulikataa ombi langu wala kunizuilia upendo wake!
Settings