Zaburi 66:13-19
13
Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa na kukutimizia nadhiri zangu:
14
nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi na nilizotamka kwa kinywa changu nilipokuwa katika shida.
15
Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono na sadaka za kondoo dume, nitakutolea mafahali na mbuzi.
16
Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu, nami niwaambie aliyonitendea.
17
Nilimlilia kwa kinywa changu, sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
18
Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, Bwana asingekuwa amenisikiliza;
19
lakini hakika Mungu amenisikiliza na amesikia sauti yangu katika maombi.
Settings