Zaburi 66:1-12
1
Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi. Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!
2
Imbeni utukufu wa jina lake; mpeni sifa zake kwa utukufu!
3
Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako! Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba adui wananyenyekea mbele zako.
4
Dunia yote yakusujudia, wanakuimbia wewe sifa, wanaliimbia sifa jina lako.”
5
Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda, mambo ya kutisha aliyoyatenda miongoni mwa wanadamu!
6
Alifanya bahari kuwa nchi kavu, wakapita kati ya maji kwa miguu, njooni, tumshangilie.
7
Yeye hutawala kwa uwezo wake milele, macho yake huangalia mataifa yote: waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake.
8
Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu, sauti ya sifa yake isikike,
9
ameyahifadhi maisha yetu na kuizuia miguu yetu kuteleza.
10
Ee Mungu, wewe ulitujaribu, ukatusafisha kama fedha.
11
Umetuingiza kwenye nyavu na umetubebesha mizigo mizito migongoni mwetu.
12
Uliwaruhusu watu watukalie vichwani, tulipita kwenye moto na kwenye maji, lakini ulituleta kwenye nchi iliyojaa utajiri tele.
Settings