Zaburi 65:9-13
9
Waitunza nchi na kuinyeshea, waitajirisha kwa wingi. Vijito vya Mungu vimejaa maji ili kuwapa watu nafaka, kwa maana wewe umeviamuru.
10
Umeilowesha mifereji yake na kusawazisha kingo zake; umeilainisha kwa manyunyu na kuibariki mimea yake.
11
Umeuvika mwaka taji ya baraka, magari yako yanafurika kwa wingi.
12
Mbuga za majani za jangwani umezineemesha; vilima vimevikwa furaha.
13
Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama, na mabonde yamepambwa kwa mavuno; vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.
Settings