Skip to content
Zaburi 63:3-8

Zaburi 63:3-8

3
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
4
Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
5
Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
6
Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
7
Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
8
Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options