Skip to content
Zaburi 63:1-8

Zaburi 63:1-8

1
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
2
Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
3
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
4
Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
5
Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
6
Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
7
Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
8
Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options