Zaburi 49:6-9
6
wale wanaotegemea mali zao na kujivunia utajiri wao mwingi?
7
Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kuukomboa uhai wa mwingine, au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.
8
Fidia ya uhai ni gharama kubwa, hakuna malipo yoyote yanayotosha,
9
ili kwamba aishi milele na asione uharibifu.