Zaburi 44:4-7
4
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
5
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
6
Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi;
7
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.