Zaburi 40:12-15
12
Kwa maana taabu zisizo na hesabu zimenizunguka, dhambi zangu zimenikamata, hata nisiweze kuona. Zimekuwa nyingi kuliko nywele za kichwa changu, nao moyo unazimia ndani yangu.
13
Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa; Ee Bwana, njoo hima unisaidie.
14
Wote wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu.
15
Wale waniambiao, “Aha! Aha!” wafadhaishwe na iwe aibu yao.
Settings