Rukia maudhui
Zaburi 37:12-20

Ushindi wa Muda Mfupi wa Waovu

Zaburi 37:12-20
12
Waovu hula njama dhidi ya wenye haki na kuwasagia meno,
13
bali Bwana huwacheka waovu, kwa sababu anajua siku yao inakuja.
14
Waovu huchomoa upanga na kupinda upinde, ili wawaangushe maskini na wahitaji, kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.
15
Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao zitavunjwa.
16
Bora kidogo walicho nacho wenye haki kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;
17
kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.
18
Bwana anazifahamu siku za wanyofu, na urithi wao utadumu milele.
19
Siku za maafa hawatanyauka, siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.
20
Lakini waovu wataangamia: Adui za Bwana watakuwa kama uzuri wa mashamba, watatoweka, watatoweka kama moshi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options