Zaburi 35:1-8
1
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami, upigane na hao wanaopigana nami.
2
Chukua ngao na kigao. Inuka unisaidie.
3
Inua mkuki wako na fumo lako dhidi ya hao wanaonifuatia. Iambie nafsi yangu, “Mimi ni wokovu wako.”
4
Wafedheheshwe na waaibishwe wale wanaotafuta uhai wangu. Wanaofanya shauri kuniangamiza warudishwe nyuma kwa hofu.
5
Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo, malaika wa Bwana akiwafukuza.
6
Njia yao na iwe giza na ya utelezi, malaika wa Bwana akiwafuatilia.
7
Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
8
maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
Settings