19
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.