Zaburi 3:3-8
3
Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4
Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5
Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
6
Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7
Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
8
Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Settings