Zaburi3
Listen to this chapter
0:00
0:00
1
Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2
Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
3
Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4
Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5
Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
6
Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7
Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
8
Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note