Zaburi 22:1-5
1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
2
Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
3
Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
4
Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
5
Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Settings