Zaburi 22:1-2
1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
2
Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.