Zaburi 20:9
Inaonyesha mstari 9 pamoja na muktadha unaouzunguka.
6
Sasa nafahamu kuwa Bwana humwokoa mpakwa mafuta wake, humjibu kutoka mbingu yake takatifu kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.
7
Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi, bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu.
8
Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara.
9
Ee Bwana, mwokoe mfalme! Tujibu tunapokuita!
Settings