Rukia maudhui
Zaburi 2:1-6

Utawala wa Mpakwa mafuta wa Bwana

Zaburi 2:1-6
1
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options