1
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”