Zaburi 144:5-11
5
Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke, gusa milima ili itoe moshi.
6
Peleka umeme uwatawanye adui, lenga mishale yako uwashinde.
7
Nyoosha mkono wako kutoka juu, nikomboe na kuniokoa kutoka maji makuu, kutoka mikononi mwa wageni
8
ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
9
Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,
10
kwa Yule awapaye wafalme ushindi, ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.
11
Nikomboe na uniokoe kutoka mikononi mwa wageni ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
Settings