Skip to content
Zaburi 137:1-6

Zaburi 137:1-6

1
Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza tulipokumbuka Sayuni.
2
Kwenye miti ya huko tulitundika vinubi vyetu,
3
kwa maana huko hao waliotuteka walitaka tuwaimbie nyimbo, watesi wetu walidai nyimbo za furaha; walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja kati ya nyimbo za Sayuni!”
4
Tutaimbaje nyimbo za Bwana, tukiwa nchi ya kigeni?
5
Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6
Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu kama sitakukumbuka wewe, kama nisipokufikiri Yerusalemu kuwa furaha yangu kubwa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options