Skip to content
Zaburi 132:1-10

Zaburi 132:1-10

1
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options