Skip to content
Zaburi 132:1-10

Zaburi 132:1-10

1
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options