Zaburi 130:5-8
5
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Settings