1
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.