Skip to content
Zaburi 124:1-7

Zaburi 124:1-7

1
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
2
kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
3
wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
4
mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
5
maji yaendayo kasi yangalituchukua.
6
Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7
Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options