Zaburi124
Listen to this chapter
0:00
0:00
1
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
2
kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
3
wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
4
mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
5
maji yaendayo kasi yangalituchukua.
6
Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7
Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
8
Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note