Zaburi 119:49-52
49
Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.
50
Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
51
Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.
52
Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.