Skip to content
Zaburi 119:41-48

Zaburi 119:41-48

41
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
42
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
43
Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
44
Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
45
Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
46
Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,
47
kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.
48
Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options