Skip to content
Zaburi 118:5-14

Zaburi 118:5-14

5
Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6
Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
8
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
9
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
10
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
14
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options