Zaburi 109:20-31
20
Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
21
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
22
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
24
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
25
Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
26
Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
27
Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
28
Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
29
Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
30
Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
31
Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
Settings