Skip to content
Zaburi 106:34-39

Zaburi 106:34-39

34
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options