Skip to content
Zaburi 106:34-46

Zaburi 106:34-46

34
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options