Zaburi 106:24-27
24
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.