Zaburi 106:19-23
19
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Settings